“Kinachovutia familia na mimi pia kila wakati ni kumgundua Kristo mara kwa mara ili kushiriki katika maisha ya maskini. Uvumbuzi huu wa ushiriki wa maskini katika miradi yetu ndiyo muda muafaka kwetu sasa. Nadhani ya kwamba, hii inatokana kulingana na mtazamo wangu, kutoelewa upatanisho unaopaswa kupatikana kati ya matajiri na maskini. Nani anapaswa kujifunza kutoka kwa nani? Ni nani anayeshikilia uzoefu wa maisha na mtazamo mwanana, muhimu kwa kufanya upya dunia, taasisi zetu, dini yetu na imani yetu?
Yesu “hashiriki”, yeye ni ushirika halisi na kutokana na mazungumzo ambayo tunayo furaha ya kushiriki, anaweza tu kuchipua, kila wakati, mwanga wa nuru ya ajabu. Nuru ambayo inashangaza, hasa kwa sababu masikini zaidi hawajapunguzwa hadi hali ya kushiriki katika wazo lililokuzwa nje yao. Wao ni wabunifu wa mawazo na hii inatokana na uzoefu wao wa umaskini uliokithiri. Bila shaka huwashangaza matajiri. Hii inaonekana kwangu kuingia katika mantiki halisi ya Injili”.
