Katika nyakati hizi ngumu, je, hatuna tabia ya kukumbuka tu matatizo yetu, na kuhesabu tu idadi ya watu wanaokwenda katika ofisi za msaada wa kijamii au wanaobisha hodi katika mashirika ya misaada?
Kwa kufanya hivyo, tunasahau hasa kukumbuka ujasiri wa familia hizi katika kuishi kwa heshima, ubunifu wao katika kukabiliana na matatizo mapya, pamoja na juhudi kubwa ambazo wanaume na wanawake wanaweka ili kupata kazi ndogo ndogo hapa na pale, kazi zisizolipwa vizuri, ngumu na hatari, na wakati mwingine zisizotambuliwa rasmi.
Tusikie mafundisho ya ujasiri, uvumilivu na heshima ambayo familia maskini zaidi zinatupatia.
Bila kufanya hivyo, tutapoteza mengi. Nyakati hizi ngumu hazitatufundisha chochote.
