Watu maskini zaidi wanaweza kuwa kichocheo cha demokrasia ya kweli.

Hali ya maskini zaidi1ni dharau kwa kanuni zetu za kidemokrasia. Hakuna demokrasia ambayo haijaegemezwa kwanza kwenye heshima kwa watu wasiojiweza. Wenye uwezo wana wajibu wa kutetea na kusaidia wasiojiweza, ili kuwaruhusu kujieleza. Vinginevyo, si chochote ila unyakuzi wa mamlaka na wenye nguvu. Tuna jukumu la kuhakikisha kwamba demokrasia zetu zinawapa wasiojiweza kila fursa ya kuwa washiriki hai., kwa msingi sawa na wenye uwezo.

Demokrasia zetu, zinazodaiwa kujengwa kwa fursa sawa, hazina usawa. Kwa karibu karne mbili, sehemu ya jamii imechukua mamlaka kiuchumi, kisiasa, kijamii, kidini. Sehemu hi haijawahi kukoma, na haikomi kamwe, bila kujali utawala wa kisiasa, ili kulinda mapendeleo yaliyopatikana na kukusanywa kwa karne nyingi.

(…)

Kimsingi ni maskini zaidi ambao wanatufunulia ukweli wa kina wa jamii zetu : Walichukua kila kitu kutoka kwao, walinyimwa usemi wowote, uwezekano wowote wa kuishi maisha ya heshima kama walivyotumaini. Waliongozwa kucheza mchezo wa wengine, wa utawala, wa misaada za hisani au za kijamii. Wamegeuzwa kuwa vitu, si wahusika wa ufahamu, ambao wana fursa ya kutoa sauti zao wenyewe. Walilazimishwa kutenda, kusema uwongo, “kuiga” ili kupata njia fulani za kuishi.

Hata hivyo, unapofahamiana na familia hizi, kila wakati unashangazwa na thamani ya kibinadamu unazopata ndani yao. Kwa maana mwanadamu hakubali kusagwa wala kuchanganywa; mwanadamu hupinga.

Kama mwanamume yule niliyekutana naye huko Jura. Alipoteza kazi kwa sababu nzito, na sasa, hatawahi kupata mwingine katika eneo hilo. Hapa kuna familia ambayo, kwa sababu ya jamii – na jamii hii ni sisi – haijui jinsi ya kusaidia walio wake, jinsi ya kuwaruhusu kuishi, imejikuta imepotea, hayawezi kulea watoto wake wanne isipokuwa kwa uporaji na kuombaomba.

Hata hivyo, mwanamume huyu ni mchapakazi. Nimemjua kwa miaka 12. Alikuwa akipata kazi, akiupoteza, alikuwa akiendelea kufuatilia bila kuchoka hadi apatapo mwingine. Juzi, nilipoingia nyumbani kwake, mwanamume huyu alikuwa ameegemea meza ya jikoni. Akajinyoosha, akanipokea kwa heshima, alinieleza kuhusu shida zake, matarajio yake, na hamu yake kubwa ya kufanya kazi.

Hivyo ndivyo hali ya chini kabisa ya wafanyakazi maskini inavyokuwa: ulimwengu wa wafanyakazi ambao wamesukumwa kwa muda mrefu kufanya kazi duni tu. Kwa sababu hali yao ilionekana kuwa duni, walipewa elimu duni, na hapa kuna mrithi wa watu hawa ambaye hana kazi, akiwa na umri wa miaka 35, na ambaye, mwishoni mwa meza yake, kwa nafsi yake yote ananililia: nitafutie kazi!

 

  1. Katika maandishi ya asili, Padre Joseph anazungumzia hali ya tabaka la chini kabisa la wafanyakazi, neno ambalo lilisikika wakati huo na katika muktadha wa Magharibi, lakini ambalo leo halina nguvu ile ile ya kueleweka..
0 comments Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.